Tuesday, December 18, 2012

ROSE MUHANDO KUPAGAWISHA IRINGA KRISMAS UWANJA WA SAMORA.......deejay jona

Mwimbaji nguli wa nyimbo za injili nchini Tanzania na Afrika Rose Muhando anatarajiwa kuwapagawisha wakazi wa mkoa wa Iringa katika tamasha kubwa lililopewa jina la mlipuko wa lulu za injili likakalofanyika siku ya jumanne ijayo katika skikukuu ya ya Krismas kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa.

Mratibu mkuu wa tamasha hilo Victor Chakudika ambae ni meneja wa kituo cha |radio Nuru Fm Iringa amesema kuwa maandalizi yote kwa ajili ya tamasha hilo yamekamilika na kuwa zaidi ya wasanii sita kutoka nje ya mkoa wa Iringa na ndani ya mkoa wa Iringa watashiriki kutoa burudani katika tamasha hilo.

Chakudika alisema kuwa tamasha hilo ni maalum kwa wakazi wa mkoa wa Iringa katika kusherekea sikukuu ya Krismas na hivyo kuwataka wapenda burudani wote mkoani Iringa badala ya kwenda katika kumbi za miziki ya kidunia kwa siku hiyo kuweza kuungana na wakristo kote duniani katika kusherekea kuzaliwa kwake Yesu Kristo .


Hata hivyo alisema kiingilio ambacho kimewekwa kwa ajili ya tamasha hilo ni kidogo zaidi kwa ajili ya kuwawezesha watu wote kuweza kukusanyika pamoja na kupokea baraka za Mungu kupitia mwimbaji huyo Rose Muhando na wengine wengi ambao wataongozana na mwimbaji huyo.
ROSE  MUHANDO  KUPAGAWISHA  IRINGA KRISMAS UWANJA  WA  SAMORA 

Mwimbaji nguli wa nyimbo  za injili nchini Tanzania na Afrika  Rose Muhando anatarajiwa  kuwapagawisha   wakazi  wa mkoa  wa Iringa katika tamasha  kubwa lililopewa  jina la mlipuko  wa lulu za injili likakalofanyika siku ya jumanne ijayo katika skikukuu ya ya Krismas kwenye  uwanja  wa Samora mjini Iringa.

Mratibu mkuu  wa tamasha  hilo Victor Chakudika ambae ni meneja  wa  kituo cha |radio Nuru Fm Iringa amesema  kuwa maandalizi  yote kwa ajili ya tamasha hilo yamekamilika na  kuwa  zaidi ya  wasanii sita kutoka nje ya mkoa wa Iringa na ndani ya mkoa  wa Iringa  watashiriki  kutoa burudani katika tamasha  hilo.

Chakudika alisema  kuwa tamasha  hilo  ni maalum kwa  wakazi  wa mkoa  wa Iringa katika  kusherekea  sikukuu ya Krismas na hivyo  kuwataka  wapenda  burudani  wote mkoani Iringa badala ya kwenda katika kumbi za miziki ya kidunia kwa  siku  hiyo  kuweza kuungana na  wakristo  kote  duniani katika kusherekea  kuzaliwa  kwake Yesu Kristo .


Hata  hivyo  alisema  kiingilio ambacho  kimewekwa kwa ajili ya tamasha  hilo ni kidogo  zaidi kwa ajili ya kuwawezesha  watu  wote  kuweza  kukusanyika pamoja na kupokea baraka  za Mungu  kupitia mwimbaji  huyo Rose Muhando na wengine wengi ambao  wataongozana na mwimbaji huyo.

No comments: