Friday, January 11, 2013

NA Beyonce aonesha 'her sexy body' kwa pozi matata kwenye jarida la GQ..asema yeye ni alama ya mafanikio ya wanawake duniani, angalia picha zake hapa

Baby's mama wa Jay-Z, the queen herself Beyonce Knowlence amepata deal ya kulipamba jarida la GQ kwa picha kadhaa zinazoonesha mwili wake wenye mvuto licha ya kuwa hivi sasa ni mama wa mtoto mmoja.
Beyonce ameliambia jarida hilo kuwa anafurahia sana kuona kuwa ameweza kuzifikia ndoto zake za kuwa alama ya mafanikio na uwezeshwaji wa wanawake duniani, lakini anapata ugumu wa kujua ni kiasi gani ameweza kuwa-influence wanawake hao.

Muangalie Queen Beyonce na pozi matata, bado anakimbiza sana tu:
Mama Blue Ivy alifunguka zaidi, "Wakati naandika nyimbo za Destiny's child, kilikuwa kitu kikubwa sana kwangu kuwa mdogo vile na kuweza kucontrol. Na lebel yetu kwa wakati ule haikujua kama tungekuja kuwa na mafanikio kiasi kile, kwa hiyo walitupatia nafasi ya kujicontrol. Na nikaiweza. Ni lengo langu katika maisha yangu kuwa mfano wa namna hii.
Alipoulizwa kama anajua kuwa ana nguvu nyingi katika ulimwengu wa wanawake alijibu, "Najua hilo, ndio, nina nguvu. Nina nguvu zaidi hata ya akili yangu inavyoweza kuchanganua na kuelewa.

No comments: