Wednesday, March 13, 2013

RAY, KING MAJUTO, JB NA IRENE UWOYA WAFUNIKA RWANDA.



HAPA NI IRENE UWOYA NA KWA NYUMA NI KING MAJUTO WAKIFATILIA HIZO TUZO KWA UMAKINI KABISA
WAIGIZAJI nguli katika tasnia ya filamu hapa Tanzania, Ray, JB, King Majuto pamoja na Irene Uwoya wamefunika mbaya katika tamasha la utoaji tuzo huko nchi Rwanda ambapo msanii kama Irene Uwoya ilibidi jina lake la asili lipotee na kujikuta akikumbushwa enzi za nyuma alivyotesa katika filamu iliyotamba na kuwa gumzo ya Oprah on Sunday.

Matangazo katika redio televisheni jina lilokuwa likisikika ni Oprah umugore wa Katawuti wakimananisha kuwa Irene mke wa mchezaji wa mpira Ndikumana, jina la Oprah limekuwa ni jina maarufu nchini Rwanda kufuatia filamu ya Oprah on Sunday iliyowashirikisha wasanii nyota marehemu Steven Kanumba na Vincent Kigosi ‘Ray’.

Wanyarwanda walilipuka ukumbi huku wakiita Oprah na Ray wakimwita Kigozi badala ya Kigosi, tuzo hizo zilizopewa jina la Rwanda Movie Awards zikilenga kuwatunuku wasanii wa filamu wa nchi hiyo na wasanii kutoka Bongo wakiwa kama watu mashuhuri waliofika kutoa zawadi kwa washindi walichaguliwa Rwanda Movie Awards.

JB NA RAY WAKIPEANA MAWILI MATATU


RAY


RAY, IRENE & KING MAJUTO

No comments: