Friday, November 28, 2014

DULLY AELEZA SABABU YA KUACHIA WIMBO WAKE ULIOJAA MATUSI

Siku chache baada ya wimbo wake wa Thats The Way uliojaa matusi yasiyoweza kuandikika kuanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao , msanii wa kitambo wa muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amefunguka kuwa halikuwa kusudio lake kuachia wimbo huo bali ulivuja kwa bahati mbaya mitandaoni.

Akipiga stori na Djjonamusic Blog hivi karibuni, Dully alisema kuwa wimbo huo aliomshirikisha mwanadada Maunda Zorro, aliurekodi miaka nane iliyopita kwenye studio yake ya Dhahabu Records na hakupanga kuutoa lakini kwa bahati mbaya ukavuja na kuingia kwenye mitandao.

No comments: