Tuesday, November 11, 2014

Mkasi | S10E07 With Miss Tanzania 2013/14 – Happy Watimanywa

Waliposema “Beauty with the Brain”, hawakukosea. Na zaidi wakagonga kwenye kiini walipompa taji hilo Miss Tanzania 2013, Bi Happyness Watimanywa. Happy, kama ambavyo walio karibu nae hupenda kumuita, ndie mwakilishi wa Tanzania katika Miss World 2014, baada ya kubadilika kwa kalenda ya uwakilishi wa Kitanzania kwenye mashindano hayo ya Unyange duniani, ambapo sasa mshindi anapata muda wa kutosha kujiandaa.
happy watimanywa
Aliitika wito wa Mkasi TV, na tulipata wasaa wa kipekee kuzungumza nae. Akiwa binti mchanga kabisa wa miaka 20, mengi yaliyosikika kutoa kwake yalionesha upeo na ukomavu wa kiakili. Lakini zaidi, yalithibitisha kuwa mtoto anapokulia kwenye mazingira yenye upeo, na hukua kiakili mapema.
Happy ni mmoja kati wa vijana wa Kitanzania waliopata nafasi za kusoma na kuhitimu katika shule moja ya Kitamaifa nchini, na katika masomo yake kuna mafanikio mengi, moja likiwa kuwa mmoja kati ya wanafunzi waliofanya vema sana kwenye somo la Uhasibu, katika mtandao wa Shule za Sekondari za Kimataifa. Mahiri kwenye lugha, na akiwa na historia ya kutembelea nchi mbali mbali, ni dhahiri huyu ni Miss Tanzania wa kipekee.
Akiwa ana matarajio ya kuendelea na masomo endapo hatofanikiwa kutwaa taji la Miss World, Bi. Happy anabeba bendera ya Tanzania kwa matumaini makubwa ya kuliwakilisha taifa vema. Taifa nalo lina nafasi na wajibu wake kumpa sapoti anayohitaji kufanya vema.

No comments: