Monday, October 12, 2015

The Game adai kuwa alirekodi nyimbo 700 kwa ajili ya Album yake mpya ‘The Documentary 2″

Rapper The Game amedai kuwa alirekodi nyimbo 700 kwa ajili ya album yake mpya “The documentary 2′ lakini aliamua kupunguza baada ya kushauliwa na Dr.dre.
 
Akifanya mahojiano na kipindi cha ‘Skee’s talk show’ The Game amesema aliamua kupunguza nyimbo hadi 38 baada ya kumsikilizisha Dr.dre nyimbo 20 lakini akazipondea zote.
 
 Album ya The Documentary 2 inatoka kwa mfumo wa Disc one na two ambao disc 1 yenye track 18
imetoka tarehe 9 October mwaka huu na Disc 2 itatoka tarehe 16 mwezi October, Album hii imeshirikisha wasanii wakubwa ikiwemo  Dr. Dre, Ice Cube, Q-Tip, Diddy, Nas, Busta Rhymes,Snoop Dogg, E-40, Scarface, DJ Quik, will.i.am, Kanye West, Lil Wayne, Kendrick Lamar, Schoolboy Q, Ab-Soul, Jay Rock, Drake, DeJ Loaf, Future, YG, Problem, Ty Dolla $ign and Jelly Roll na wengine.

No comments: