Mashabiki Wanataka Kuendesha Muziki Kitu Ambacho Sio Sawa – Mwana FA
Mwana FA amewataka mashabiki wa muziki
nchini kuacha tabia ya kuwalazimisha wasanii wa muziki kufanya kila kitu
wanachokitaka hata kikiwa hakina mantiki kwa wakati huo.
Rapa
huyo aliyeachia video ya wimbo ‘Asante kwa Kuja’, amekiambia kipindi
cha 360 kinachoruka Clouds TV kuwa msanii ndiye anayetakiwa kumbadilisha
shabiki kwa kumpatia vitu tofauti. “Mashabiki wanataka

kuendesha muziki
kitu ambacho sio sawa na sio sahihi,” alisema FA.
“Ukienda
kule kwenye page za Instagram ambako mashabiki wanaweza kukufikia
kiurahisi unaweza ukapata lawama kwanini haubadiliki una sound kama old
school rapa au mwingine anataka ubaki kama ulivyokuwa unarap zamani bila
kujua sasa hivi tupo mbele zaidi.”
“Muziki
sio kama ni jiwe tuuchukulie kama mti unakuwa na kuna changes
zinatokea. Lazima tubadilike ukiangalia video zangu sidhani kama unataka
nifanye tena video kama ya ‘Mabinti’. So ni lazima watu wakue, dunia
inaenda kasi na muziki unakuwa ni lazima ubadilike. Kwahiyo mtu
akiniamba hataki nibadilike anataka nibaki nilivyokuwa, sielewi,”
alisisitizia FA.
No comments:
Post a Comment