Monday, September 24, 2012

Kanumba na Lulu waliitana Mopao na Cindy … unajua maana yake?

image
Ukifuatilia Tweet Page za Kanumba na Elizabeth Michael aka Lulu utaona kuwa walijaribu kutumia majina ya Mopao na Cindy labda kunogesha chat yao au katika kupoteza maboya wafuasi wao kwenye mtandao huo wa kijamii au labda kujifananisha na nguli ambaye Kanumba mwenyewe aliwahi kukiri kuwa anampenda sana Koffi Charles Olomide Mopao Sakonzy, huku Kanumba akimuita Lulu Cindy na Lulu akimuita Kanumba Mopao.
Kanumba alikuwa mpenzi mkubwa sana wa Bolingo na jina la Mopao ni jina la Koffi Olomide ambaye mashabiki wanamuita Mopao Mokonzi. Koffi amekuwa kwenye uhusiano wa kimapaenzi na muimbaji wake wa kike anayejulikana kwa jina la Cindy Le Coeur ambaye kwa sasa ndiye mke wake kipenzi. Koffi wakati akiaanza uhusiano na Cindy ilikuwa ni siri na iliandikwa sana kwenye vyombo vya habari lakini kila mara walipoulizwa walikana mpaka kwenye Birthday ya Cindy ndipo Koffi alipovunja ukimya na pale alipomzawadia gari aina ya Jaguar baba yake na Cindy (Gonga hapa kuisoma) na mpaka wa leo Cindy ambaye anakuja kwa kasi kwenye wanamuziki wa kike na amejizolea umaarufu kwa nyimbo zake za Koffi Chante Cindy ambapo amekuwa akizirudia nyimbo za taratibu za Koffi tangu enzi hizo.
Sasa baada ya kukueleza hayo soma Tweet za mwisho za Kanumba “Mopao” na Lulu “Cindy”.
image
image
image


Compilation ya Tweet hizi ni kwa hisani ya Shafi Dauda Blog.
Mamaa Cindy Olomide..............posted by deejay jona

No comments: