Saturday, December 22, 2012

‘Fungua Mwaka 2013 La Weusi’ jumapili hii Maisha Club, Lord Eyez kuwasapraiz fans wake, Wataizindua DVD ya Kum Kubam, waahidi kupiga ‘Show ya Milele’.


‘WEUSI’ jina ambalo limefunika sana kwenye playlist za media mbalimbali kwa mwaka huu, sasa wameamua kuufunga mwaka kwa aina ya pekee, ambapo wanatarajiwa kupiga show kali ya kuufunga ukurasa wa mwaka huu Jumapili hii(December, 23) pale Maisha Club.
Lord eyez atawasapraiz fans wake kama alivyowaahidi kwenye press conference aliyoiitisha hivi karibuni baada ya matatizo aliyopata, ambapo ngoma yake mpya ya
‘Mapito’ inayosubiriwa kwa hamu itasikika usiku huo.
Kitu kingine kikubwa ni uzinduzi wa DVD ya Nikki wa Pili ‘Kum Kubam’ jina ambalo limesumbua pia kwenye zile ngoma zenye element zote za Hip Hop.
Mweusi G-Nako ameiambia Leotainmenttz.com  kuwa sababu za kuliita ‘Funga Mwaka la Weusi’ ni matukio makubwa yatakayofanyika usiku huo, uzinduzi wa wimbo wa Lord Eyez ambao unasubiriwa kwa hamu, Uzinduzi wa DVD ya Kum Kubam, na kwa mara ya kwanza watu watashuhudia aina mpya ya usambazaji wa kazi za wasanii. Hii ni aina gani tena? Tutaifahamu tu jumapili.
G-Warawara amewaahidi fans wao kuwa watashuhudia ‘show ya milele’ toka kwa safu ya WEUSI, JOH MAKINI, NIKKI WA PILI, BONTA, LORD EYEZ NA YEYE MWENYEWE G-NAKO.
Kiingilio katika show hiyo itakuwa sh. 10,000/- TU

No comments: