Kwa hapa bongo imekuwa kama ni story za kawaida sasa hasa
kwa wasanii wachanga kuwalalamikia wasanii wakubwa kuiba idea zao ama nyimbo
zao na kufanya hits. Huko Kenya pia imemtokea msanii wa kike aliyehustle kutoka
kuwa mfanyakazi wa ndani hadi kuwa staa.
Nyota Ndogo anatuhumiwa na msanii chipukizi wa Nchini Kenya
rapper toka mitaa ya Nairobi anaeitwa Kachela Kroma, na wimbo ambao unaleta
haya yote unaitwa 'Tunataka Amani'.
Kachela alifunguka kuwa aliandika wimbo huo baada ya
machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, na akaurekodi wimbo huo
na msanii mwenzake anaeitwa Bunsen B katika studio iliyoko Nairobi ambayo kwa
sasa inaitwa Ketebul Music enzi hizo ilikuwa inaitwa Ketebu Production na
producer mtanzania mwenyeji wa Mwanza Jesse Bukindu ambae hivi sasa ni rafiki
wa karibu wa Nyota ndogo.
Rapper huyo chipukizi amemrushia mpira wa lawama producer
Jesse kuwa alikuwa na tabia ya kuucheza wimbo huo mara kwa mara na
kuwasikilizisha watu mbalimbali waliofika pale studio akiwemo Nyota Ndogo na
hapo ndipo anaamini Nyota ndogo aliukwapua na kuuweka kichwani.
No comments:
Post a Comment