Wednesday, November 12, 2014

Top 5 ya watangazaji wanaozitengenezea Media zao mkwanja mrefu zaidi hapa Tanzania

Nafasi tano za watangazaji wanaozitengenezea media zao mkwanja wa kutosha na kufanya redio kujulikana zaidi na kuwasogeza wasikilizaji wengi zaidi na kumshawishi mdau kuweza kutangaza na redio husika.

Utaratibu huu utakua ni kwa kila j5 ya kila wiki na hii idea ni ya kwanza kabisa katika ulimwengu wa blog hapa Tanzania sio mbaya kama ukiona inafaa na kuindeleza kwenye chanzo chako Team Djjonamusic blog na Radio imekaa chini na kuona bora kuanzisha hizi chati.

 
Nafasi ya tano imekamatwa na Dokta joe huyu jamaa ni mtangazaji wa kituo cha redio cha Ebony fm iliyopo mkoani Iringa, jamaa anaendesha show inaitwa The splash hii show huluka kuanzia jumatatu mpaka ijumaa time ni saa saba na robo mpaka kumi kamili.


Nafasi ya nne imeshikiliwa na Fadhili haule ambaye ni mtangazaji wa redio Times fm  iliyopo hapa Dar na show ambayo anaiendesha inaitwa Sunrise ni kila siku za wiki namaanisha j3 mpaka ijumaa.

Nafasi ya tatu imeshikiliwa na Renatus Bizzo kiluvia ambaye ni mtangazaji wa Redio free Africa iliyopo jijini mwanza show inaitwa Showtime New chapter ni kila siku za wiki.

Nafasi ya pili imeshikiliwa na Julias Kamafa uyu jamaa ni mtangaza wa redio 5 iliyopo njiro Arusha show anayoiendesha inaitwa Funiko Baze ni kila siku za wiki j3 mpaka ijumaa.

 

Na kwa hii wiki nafasi ya kwanza imeshikiliwa na B12 aka The navigator wote mnafaham uyu jamaa yupo pale Clouds fm show inaitwa XXL time saa saba kamaili mpaka kikumi kamili.

No comments: