Monday, June 8, 2015

Blatter Adaiwa “kuchepuka” na ‘ex’ wa Cristiano Ronaldo.

Rais wa FIFA aliyetia aibu Sepp Blatter ametajwa kuwa mpenzi wa zamani wa mwanamitindo Irina Shayk ikiwa ni kisa kinachotikisa vichwa habari duniani kote. Gazeti la kila siku la Hispania la El Mundo limechapisha madai hayo kuhusu mkuu huyo wa soka mwenye macho makali na mpenzi wa zamani wa Cristiano Ronaldo katika habari iliyochapishwa jana ikiwa na kichwa “Wanawake wote katika maisha ya  https://igcdn-photos-b-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xaf1/t51.2885-15/11385589_373340289538121_1517585793_n.jpgSepp Blatter.” Ilitangazwa kuwa babu huyo, 79, alikuwa na uhusiano na mrembo huyo wa Urusi baada ya kuwa na mahusiano na mcheza tennis Ilona Boguska lakini kabla hajakutana na mlimbwende Linda Barras, 50. Blatter alianza kumuona mzaliwa wa Poland Ilona, rafiki wa binti yake Corinne, mwana 1995 ambapo waliachana mwaka 2002, inavyodaiwa. Walirudiana tena baada ya ndoa fupi ya Blatter mwaka 2002 na Graziella Bianca – mkufunzi wa pomboo ambaye pia alikuwa rafiki wa binti wake.

No comments: