Tuesday, June 9, 2015

SHOCKING!! Kumbe JOKATE Ashawai Taka Kujitia Kitanzi.

Sexy lady Mtafutaji Anayejishughulisha na fani lukuki ikiwemo urembo na muziki, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kwa mara ya kwanza ameweka wazi kwamba alitaka kunywa sumu kisa kikiwa ni kuumizwa kimapenzi na mwanaume aliyempenda kupindukia, aya zifuatazo zimesheheni. Akizungumza na gazeti la 'Ijumaa Wikienda' , wikendi iliyopita, Jokate au ukipenda Jojo alifunguka kwamba, japokuwa haikujulikana kwa watu wa nje kutokana na usiri mkubwa uliofanywa na ndugu zake, akiwemo mama mzazi, lakini ameona ni vyema akaweka wazi ili watu wajifunze namna ambavyo mapenzi yanaweza kuharibu mustakabali mzima wa maisha ya mtu. Jokate ambaye amewahi kutajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mastaa mbalimbali Bongo 

 https://igcdn-photos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xfa1/t51.2885-15/11357549_101161650226175_166474175_n.jpg

wakiwemo staa wa mpira wa kikapu ambaye ni Mbongo anayekipiga nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka, wanamuziki, Ali Saleh Kiba na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alisema hakuona sababu ya kuendelea kuishi bila mwanaume huyo na kuona njia pekee ni kujitoa uhai. Jokate alikiri kujifungia ndani Mara kwa mara na kujaribu kunywa sumu lakini alikuwa akishtukiwa na ndugu zake hivyo kushindwa kutekeleza zoezi hilo. Alisema kufuatia hali hiyo, ilibidi awe chini ya uangalizi maalum, huku akiwa anaishi kama mfungwa na mara nyingi akipewa ushauri wa kisaikolojia na baadaye kujikuta akimfuta mwanaume huyo moyoni. “Wewe acha tu, hakuna kitu kinachouma kama mapenzi, niliumia mno, ilikuwa mbaya mno kwangu kwani nilitaka kujiua baada ya kuona kabisa siwezi kuishi bila huyo mwanaume kwa sababu nilimpenda sana tena sana. Nilijaribu kunywa sumu mara kadhaa lakini nilikuwa naokolewa na ndugu zangu, nashukuru nilipewa uangalizi maalum kutoka kwa ndugu,Unajua ukiniona huwezi kujua kama huwa naumizwa na mapenzi kwa sababu mimi ni msiri sana kwa mambo yangu binafsi kama hayo,” alisema Jokate akionekana ni mtu ambaye akipenda huwa anapenda.

No comments: