Thursday, July 16, 2015

Mo Music Baada Ya Kumaliza Chuo Aeleza Jinsi Atakavyoitumia Elimu Yake kuwekeza kwenye muziki >>>>>>

Mo Music, ni miongoni mwa wasanii wa muziki waliokuwa wanafanya vitu viwili kwa wakati mmoja, muziki na shule . Hit maker huyo wa ‘Basi Nenda’ amemaliza mitihani yake ya mwaka wa mwisho na anatarajia kuhitimu mwishoni mwa mwaka huu. “Nimemaliza mitihani sasa hivi, nilikuwa nachukua degree ya Public Relations and Markerting”Mo Music ameiambia Bongo 5. Mo ambaye amesoma katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichopo jijini Mwanza, amesema kuwa ana mpango wa kuitumia elimu aliyoipata katika
 Mo Music ( @momusic1 ) Baada Ya Kumaliza Chuo Aeleza Jinsi Atakavyoitumia Elimu Yake kuwekeza kwenye muziki >>>>>> Mo Music, ni miongoni mwa wasanii wa muziki waliokuwa wanafanya vitu viwili kwa wakati mmoja, muziki na shule . Hit maker huyo wa ‘Basi Nenda’ amemaliza mitihani yake ya mwaka wa mwisho na anatarajia kuhitimu mwishoni mwa mwaka huu. “Nimemaliza mitihani sasa hivi, nilikuwa nachukua degree ya Public Relations and Markerting”Mo Music ameiambia Bongo 5. Mo ambaye amesoma katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino kilichopo jijini Mwanza, amesema kuwa ana mpango wa kuitumia elimu aliyoipata katika kuwekeza zaidi kwenye muziki wake.“Kitu kikubwa nashukuru Mungu kwamba kazi ninayoifanya muziki na kile nilichokisoma vinakuwa vinakutana yaani vinashabihiana, kwasababu nimesomea Public Relations and Marketing, Public Relation ndio ni kudeal na mahusiano na watu mbali na hapo Marketing ndio biashara yenyewe kwa hiyo ina maana muziki wangu nitaufanya zaidi kisomi pasipo kukurupuka, kwa hiyo nita-invest zaidi katika muziki wangu kama biashara kubwa.”Ameongeza kuwa hana mpango wowote wa kuajiriwa kwa sasa, na hata ikitokea fursa labda itakuwa kwa baadae.“Mimi moyo wangu ulishakataa kuja kuajiriwa lakini itakapotokea kazi imetokea labda baadae, lakini sasa hivi nitakuwa na biashara zingine tofauti lakini kazi kubwa ambayo itakayokuwa inaniingizia kipato kwenye biashara zingine ni muziki.” Chanzo: Bongo5.co
kuwekeza zaidi kwenye muziki wake.“Kitu kikubwa nashukuru Mungu kwamba kazi ninayoifanya muziki na kile nilichokisoma vinakuwa vinakutana yaani vinashabihiana, kwasababu nimesomea Public Relations and Marketing, Public Relation ndio ni kudeal na mahusiano na watu mbali na hapo Marketing ndio biashara yenyewe kwa hiyo ina maana muziki wangu nitaufanya zaidi kisomi pasipo kukurupuka, kwa hiyo nita-invest zaidi katika muziki wangu kama biashara kubwa.”Ameongeza kuwa hana mpango wowote wa kuajiriwa kwa sasa, na hata ikitokea fursa labda itakuwa kwa baadae.“Mimi moyo wangu ulishakataa kuja kuajiriwa lakini itakapotokea kazi imetokea labda baadae, lakini sasa hivi nitakuwa na biashara zingine tofauti lakini kazi kubwa ambayo itakayokuwa inaniingizia kipato kwenye biashara zingine ni muziki.”

No comments: