Tuesday, September 22, 2015

DAVIDO amevujisha mpango wa collabo yetu mapema sana lakini sio mbaya' – Joh Makini

Joh Makini amesema kuwa mipango ya collabo kati yake na staa wa Nigeria, Davido ilianza muda mrefu lakini hakutegemea kama mwimbaji huyo wa ‘Aye’ angechukua uamuzi wa kuiweka hadharani kipindi hiki. Weekend iliyopita (Sept 18) mashabiki wa muziki Tanzania walipokea kwa furaha habari njema kuhusu ujio wa collabo ya East na West kutoka kwa Davido mwenyewe ambaye alitweet: DAVIDO X JOH MAKINI COMING SOON — Davido September 18, 2015. Joh ameiambia Djjonamusic kuwa Davido alianza kuvutiwa 
 
na kazi zake alipomshuhudia kwenye jukwaa la Fiesta, ambapo Davido pia alikuwa miongoni mwa mastaa wa Kimataifa waliotumbuiza kwenye tamasha hilo jijini Dar es salaam. “Hii kusema kweli imeanza kitambo na mchizi alikuwa ananifatilia, nakumbuka mara ya mwisho kuna show moja ilifanyika kubwa Leaders (Fiesta) na mchizi alikuwepo, sasa wakati wa performance yangu na jamaa alikuwepo, sasa kuanzia pale jamaa alikuwa ananiulizia who is this guy watu wakawa wananiambia, yaani alikuwa surprised show ilikuwa kubwa…” Ameongeza kuwa baada ya kupata feedback kutoka kwa watu mbalimbali kuwa Davido anamzungumzia vizuri na anatamani kufanya naye kazi aliamua kutumia fursa hiyo kuwasiliana naye kwaajili ya kufanya kazi. “Sasa vitu kama hivi vinapokuja inabidi na wewe ujiongeze kidogo, tukamcheki kama kuna uwezekano wa kufanya kazi na mchizi, na mchizi mwenyewe akasema alikuwa anataka sana kufanya kazi na mimi” Joh amesema kuwa tayari wameanza maandalizi ya kufanya wimbo huo licha ya Davido kuweka wazi mapema bila yeye kutarajia. “Sema yeye nafikiri amekuwa na haraka sana kuipeleka kwenye media lakini sio mbaya.” alisema Joh. Bado haijajulikana wimbo watakaofanya utakuwa ni wa nani, lakini Joh amesema inaweza ukawa wa wote wawili, lakini kazi ikishafanyika watafanya mazungumzo kuamua juu ya hilo. Hii itakuwa ni collabo ya tatu ya kimataifa kwa Joh Makini kwa mwaka huu, baada ya ile ya AKA pamojan nay a K.O ambayo nayo bado iko kwenye maandalizi.

No comments: