Tuesday, September 22, 2015

Ben Pol aipiga chini management ya Panamusiq >>>>>>>

 Ikiwa ni miezi 5 tu imepita toka Benard “Ben Pol” Paul atangaze kusaini mkataba wa usimamizi na kampuni ya Panamusiq, mwimbaji huyo wa R&B amevunja nao mkataba.Bongo5 imemtafuta Ben Pol ili kuzungumzia sababu za kusitisha mkataba huo ambao wakati wanasaini walisema ungekuwa ni wa muda mrefu (Ingia hapa ). “Unajua tumeanza kufanya kazi mwezi wa 4 na tumeachana mwezi wa 9” alithibitisha kusitisha 
 https://scontent.cdninstagram.com/hphotos-xaf1/t51.2885-15/s320x320/e35/11380249_1711926209035629_810008232_n.jpg
mkataba. Ben Pol amesema kuwa kwa kipindi cha miezi 5 ambacho amekuwa na kampuni hiyo kuanzia mwezi April hadi September 2015 alipousitisha mkataba, amekuwa akiweka rekodi ya utendaji na kwa namna fulani kuna vitu ambavyo hakuridhishwa navyo japo hakutaka kuweka wazi sababu halisi ya kusitisha mkataba. Ameongeza kuwa alikaa mezani na kampuni hiyo na pande zote mbili wakakubaliana kusitisha kufanya kazi, na kuwa wameachana kwa uzuri. Pia amesema wamekubaliana kutotoa tamko rasmi wala kuzitaja sababu za kuachana. Alhamisi ya wiki hii (Sept 24) Ben Pol ataachia single mpya ‘Ningefanyaje’ aliomshirikisha Avril wa Kenya.

No comments: