Baraza la Sanaa la Taifa
Nchini Tanzania (Basata), limeweka wazi kwamba wasanii wenye majina
makubwa ndio wanaongoza kutokuwa wanachama wa mashirikisho ya wasanii.
Baraza hilo pia limeyataka mashirikisho na vyama vyote vya wasanii nchini kufanya uchaguzi ili
Baraza hilo pia limeyataka mashirikisho na vyama vyote vya wasanii nchini kufanya uchaguzi ili

kusaidia sekta ya sanaa iwe na mfumo bora wa
utawala unaotambulika na kuheshimika na wadau, wasanii na Serikali kwa
ujumla. Katibu mtendaji wa baraza hilo, Godfrey Mungereza, alieleza hayo
jana alipokuwa katika mkutano wa majadiliano kati ya Baraza na wadau wa
sanaa nchini. Baraza hilo pia limewataka wasanii wote nchini wajisajili
ili wawe na vibali vya kazi za sanaa vitakavyowawezesha kushiriki
kikamilifu kujenga mfumo wa utawala katika sanaa ambao utatumika kama
mfumo sahihi na rasmi wa mawasiliano kati ya Serikali na wasanii.
No comments:
Post a Comment