Watu hao raia wa Kenya na watanzania watatu, akiwemo Meneja msaidizi Selestine Nalogwa Mkumbo, mtunza funguo Anastazia Frank Ringo na mpelelezi wa Bank hiyo Tegemea Ayoub ambao wamebainika kuhusika katika wizi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam Kamishna wa Polisi Kanda Maaalum ya Polisi Suleiman Kova alisema, wafanyakazi wa benk hiyo waliohusika wamekamatwa kulingana na upelelezi wa jeshi hilo na majambazi wengine walikamatwa katika eneo la Mbezi Beach wakiwa wanapanga kufanya tukio lingine la Uporaji.
Aidha kamishna Kova alisema katika upelelezi uliofanywa na jeshi la polisi umebaini kuwa zaidi ya shilingi milioni 300 zilikwisha tolewa katika benk hiyo siku chache kabla ya tukio.
Katika hatua nyingine jeshi hilo limewakamata majambazi sugu kumi pamoja na silaha mbalimbali ikiwa ni mwendelezo wa oparesheni ya kupambana na uhalifu wa kutumia silaha na pikipiki iliyoanza octoba 28 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment