Wednesday, June 24, 2015

Jack Patrick Awa Mwanamitindo Gerezani >>>>>>>>

 Mwanamitindo kutoka nchini Tanzania, Jacqueline Patrick, ambaye anatumikia kifungo chake Macau nchini China, anadaiwa kuendeleza fani yake ya mitindo akiwa gerezani na kuwa kivutio kikubwa kwa wafungwa
 
wenzake. Inadaiwa kuwa Jacqueline, licha ya kuwa gerezani amekuwa akifuatilia mitindo mipya iliyoingia mjini kisha kuwafanyia wenzake jambo ambalo ameonesha kuungwa mkono kutokana na talanta aliyokuwa nayo. Inadaiwa kuwa kutokana na kipaji hicho amejikuta akimwagiwa sifa kemkem na uongozi wa gereza hilo akiwa anatumikia kifungo hicho baada ya kupatikana na hatia ya kujihusisha na biashara haramu ya
madawa ya kulevya. Jack Patrick alishawai kutokea Kwenye Music Videos Kadhaa za Bongo Flava kama 'Video Vixen'

No comments: