Saturday, June 27, 2015

Ommy Dimpoz Ataja Umuhimu wa Meneja kwenye muziki wake >>>>>>

 Ommy Dimpoz amesema mafanikio makubwa aliyonayo na kuweza kupenya kwenye ‘mainstream’, yametokana na kuelewa nini umuhimu wa kuwa na msaidizi na msimamizi katika kazi zake na kumpa shavu meneja wake, Mubenga. Ommy Dimpoz ameiambia E-News ya EATV kuwa alikuwa na mambo mengi ya kufanya ambayo kama isingekuwa meneja asingeweza kuyafanya yote. “Nilipoamua kufanya kazi kama solo  Ommy Dimpoz ( @ommydimpoz ) Ataja Umuhimu wa Meneja kwenye muziki wake >>>>>> Ommy Dimpoz amesema mafanikio makubwa aliyonayo na kuweza kupenya kwenye ‘mainstream’, yametokana na kuelewa nini umuhimu wa kuwa na msaidizi na msimamizi katika kazi zake na kumpa shavu meneja wake, Mubenga.  Ommy Dimpoz ameiambia E-News ya EATV kuwa alikuwa na mambo mengi ya kufanya ambayo kama isingekuwa meneja asingeweza kuyafanya yote. “Nilipoamua kufanya kazi kama solo artist niliona umuhimu wa meneja maana mwanzo kuna changamoto nilikuwa nazipata kama kufuatilia kazi zangu mwenyewe,” amesema muimbaji huyo wa Wanjera. “Nilikuwa napata ugumu kipindi hicho maana nilikuwa sina hata usafiri, nilikuwa napanda daladala. Unajua foleni njiani unakuta hadi nilikuwa nachelewa mazoezi. Kipindi hicho nipo katika band ndio maana nilivyoamua kuwa solo artist nilitambua hilo ndio maana nikaamua kuongea tena na Mubenga ndio hadi nikatoa wimbo wa “Nai Nai” pale tayari nilikuwa na nguvu ya meneja,” aliongeza.  Chanzo: Bongoartist niliona umuhimu wa meneja maana mwanzo kuna changamoto nilikuwa nazipata kama kufuatilia kazi zangu mwenyewe,” amesema muimbaji huyo wa Wanjera. “Nilikuwa napata ugumu kipindi hicho maana nilikuwa sina hata usafiri, nilikuwa napanda daladala. Unajua foleni njiani unakuta hadi nilikuwa nachelewa mazoezi. Kipindi hicho nipo katika band ndio maana nilivyoamua kuwa solo artist nilitambua hilo ndio maana nikaamua kuongea tena na Mubenga ndio hadi nikatoa wimbo wa “Nai Nai” pale tayari nilikuwa na nguvu ya meneja,” aliongeza.

No comments: