Monday, June 22, 2015

Shilole: Kingereza sio lugha yangu, nimekosea au nimepatia vyote sawa tu.

Msanii wa kike wa muziki wa kizazi kipya anayeiwakilisha vyema Igunga, Zuwena Mohameid “Shilole” amesema Kingereza si lugha yake kwa hiyo kukosea au kupatia kuzungumza haina tatizo kwake.
Akizungumza kupitia kipindi cha “The playlist” cha “Times fm”, shilole amedai haoni sababu ya yeye
 
kujifunza Kingereza kwa kuwa sio lugha ambayo amekuta ikizungumzwa Tanzania.
“Mimi kingereza sio lugha yangu, mi nafanya tu nikipatia sawa nikikosea tu sawa, nikikosea Kiswahili waseme tu nakosea hadi Kiswahili, lakini kingereza sio lugha yangu kwa hiyo naongeaga basi tu sio lazima” alisema Shilole.

Kwenye line nyingine mmiliki huyo wa “malele”, amedai ndoto zake za kugombea Ubunge Igunga oktoba mwaka huu zipo kama kawaida, anachofanya kwa sasa anataka akomae kisiasa na “soon” atatangaza kuanza harakati hizo.
Credit:timesfmtz.com

No comments: