Wednesday, June 17, 2015

Wastara ‘awachana’ wanasiasa >>>>>>>

 Msanii wa filamu nchini Tanzania, Wastara Juma, amedai kuwa wanasiasa wanawatumia sana wasanii katika kampeni zao na baada ya kufanikiwa wanawasahau na kuwaona ni wasumbufu pale wanapohitaji msaada. Amesema kuwa kipindi wanasiasa wakiwa wanauhitaji nao huwaona kama lulu na kuwatumiwa ipasavyo  lakini mchakato ukiisha kuwaona kuwa hawafai, kitendo ambacho amedai sio kizuri kwani wanatakiwa kukumbukwa wakati wote na sio katika shida tu. Amedai kuwa kwa upande wake hapendi siasa wala hapendi kufungamana na mtu kwa kuwa wasanii wanatumiwa sana muda huu kwa kuwa wanashida, na kudai kuwa baada ya hapo wanawaacha solemba na wakihitaji msaada kusaidiwa jambo lenye maslahi huenekana wasumbufu.

No comments: