Rapper mkongwe, Earl Simmons aka Dark Man X amemtupia lawama meneja
wake wa zamani kwa kutofanya wajibu wake ipasavyo hivyo kupelekea
rapper huyo kuwekwa chini ya ulinzi kwasababu ya kutolipa pesa ya malezi
ya watoto wake.
DMX ambaye hivi karibuni amerudi studio kwa ajili ya kutengeneza
Album mpya, amedai kuwa suala hilo lilitakiwa liendeshwe kibiashara na
meneja wake ndio alitakiwa alipe kwasababu anamfahamu mwanamke huyo
ambaye ni mama wa watoto wanne kati ya 12 wa rapper huyo.
DMX aliwekwa chini ya ulinzi wiki iliyopita muda mchache baada ya
kutoka jela kwakosa hilohilo la kutolipa pesa ya malezi kwa muda, Hata
hivyo DMX ameachiwa huru na kesi hiyo imesogezwa hadi November 18.
Wakili wa DMX, Jeffrey Chartier amesema “Lengo pekee hivi sasa ni kufanya kazi na kutimiza majukumu yake, na hii inampa fursa nzuri ya kufanya hivyo”
No comments:
Post a Comment