Mitandao imekuwa kwa kiasi kikubwa sana,kila mtu anatumia account
yake vile anavyojisikia, tukiacha Twitter,Instagram na Snapchat,
Facebook ni mtandao unaotumika sana na ni kwasababu ni rahisi kutumia
kuliko mitandao mingine, idadi ya watumiaji inaongezeka siku hadi siku
vijana wadogo hata
![](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_tKSJ4WQEjlVRXJnuzhZQ-F4IyC-4JPFDCcGdm5oUf7wOfvBd4uYkxU0d4F0-Ewl_lj_AfONGnZTwZyiuoaDI8iy7XiEsCNIw_u-STXv29UQOiaigFuqv-9d-BzTl2tYMCVv8hPdXb9DbG1aXRt0_1pfidgpdaHVyZkXxOB2z-CQN1fav7e9f0yBK28MtHsjGyrfhJ-6C7x7geesM8GNPm6Wjk=s0-d)
wa shule za misingi nao wanajua kutumia mtandao huu,
lakini je tunatumia mitandao vizuri inavyotakiwa au tunajua nini madhara
ya kutumia mitandao ndiyo sivyo.
Kuna mambo ya kuzingatia unapo post vitu katika ukurasa wako wa
facebook leo nitaongelea vitu saba muhimu ambavyo kila siku tunapost na
hatujui kama inaweza ikawa tatizo kwetu hasa kwa usalama wa kwetu na
familia zetu .
- Anuani ya Nyumbani Kwenu/kwako
Wapo watu wanapiga picha nje ya mageti ya nyumbani kwao,wakati
mwingine unapiga hata number ya nyumba yenu na hujui, watu kitu ambacho
hawajui hizo taarifa unazoweka katika mtandao zinaweza onekana na watu
wengi hata wale ambao sio marafiki zako hii ni hatari kwa usalama wako
na gamilia yako na wakati mwingine inaonekana kama ni kitu cha kawaida
sana ila miaka inavyozidi kwenda mitandao inakuwa na tekinologia pia na
uhalifu pia utaongezeka.
- Taarifa za Ofisini kwako.
Kuandika unafanya wapi kazi pia ni tatizo, kama wapo watu wenye nia
mbaya na wewe wanaweza kukufwatilia kwa kufwata tu taarifa zako za
ofisi. Kama nilivyosema tekinologia inakuwa kwahiyo kitu cha muhimu
kufanya ni kuhakikisha unaficha taarifa zako za karibu sana ambazo sio
lazima watu wote wazione.
- Namba Yako ya Simu
Wapo watu wanaandika namba zao za simu kwenye taarifa za kuwahusu
kwenye profile zako, unaweza kupigiwa simu na watu wengi wasio na maana,
na hii wengi imewakuta wanapigiwa na watu hawawajui. Tumefikia wakati
watu hatuaminiani na huarifu ni mwingi kwahiyo ni vizuri ukatoa namba
yako ili isionekane na kila mtu.
- Mahusiano yako.
Kuna vitu sio muhimu kama kubadili status kutoka single kwenda
kwenye Relationship au engaged au married sio ishu sana, haijalishi
utapata watu wangapi watakao comment kwenye profile yako, maisha yako
yawe private kwako sio lazima kuonyesha dunia nzima unatoka na nani
japokuwa hii ni fashion kwa watu wengi na kama hujampost mpenzi wako kwa
wengine inakuiwa tatizo.
- Malipo yako.
Baadhi ya sifa zinaweza kuwaua watu, mtu kapata cheki ya pesa nyingi,
basi ataipost facebook wapo watu wanapost pesa nyingi sana kwenye
mitandao hii inaweza ikawa ni hatari kwako na watu wanao kuzunguka
watu wanajifunza kutumia vizuri mitandao ikiwewo jinsi ya kutract mtu
kutumia taarifa zake anazo tuma kwenye mitandao hii inaweza ikawa si
sawa kwa usalama wako.
- Picha za Utupu
Kutuma picha za utumu ni tatizo, wapo watakao zitumia vibaya na hii
itakupa sifa mbaya kwa jamii kwa wadada msijaribu kuwa kama kim
kardashiana yeye anaweza kupata pesa nyingi kwa picha moja tu ya matiti
yake. Mnatakiwa kujielewa na kama umeamua kufanya biashara kumbuka kuna
sheria ya mitandao siku hizi.
- Hali yako na unavyojisikia.
Haina haja ya kusema kila unachojisikia kusema, japokuwa uhuru ni
wako, kuna mambo mengine yanaweza kuwa siri yako, wapo wanaotumia
mitandao ya kijamii kama diary ambayo anaandika kila kitu kuhusu maisha
yake, usifanye watu wakusome maisha yako yote kwa kutumia tu ukurasa
wako wa facebook.
No comments:
Post a Comment