Wednesday, November 11, 2015

Picha: Alikiba akutana na Fergie wa The Black Eyed Peas na Nikita Los Angeles Marekani

Mkali wa ‘Chekecha cheketua’ KingKiba aka Alikiba amekutana na Fergie  mmoja wasanii wanaounda kundi la Black Eyed Peas na Maggie Q muigizaji wa Tamthilia ya ‘Nikita’ Los Angeles, Marekani.

Fergie mbali ya kuwa muimbaji pia ni muigizaji, mtangazaji wa mwanamitindo, aliapata mafanikio makubwa na kundi la Black Eyed Peas lililowahi kutamba na vibao kama ‘Boom boom pow’ na ‘I got a feeling’
maggie q                                        Alikiba akiwa na Maggie Q
Maggie Q ni mwanamitindo na muigizaji wa Tamthilia maarufu ya ‘Nikita’ pia ameigiza kwenye tamthilia iliyoanza kuoneshwa mwaka jana ya ‘Stalker’ na pia ameigiza kwenye filamu nyingi ikiwemo Divergent iliyotoka mwaka jana pia.
Alikiba yupo Los Angeles Marekani ambapo ameenda kwa ajili ya kushoot video yake mpya na kwa ajili ya Kampeni ya Wild aid ambapo yeye ni moja ya mabalozi wa kampeni hiyo.

No comments: