Msanii wa Bongo Fleva , Hamis Mwinjuma aka Mwana FA amesema pamoja na kwamba tasnia ya muziki inabadilika, hawezi kuwaunga mkono wasanii wanaopoteza misingi ya muziki wa Hip Hop kwa kivuli cha kutengeneza pesa.
“Iko so obvious muziki umebadilika sana, umetoka katika ile misingi iliyowekwa na sababu zake za kuwepo, umekuwa kuhusu starehe na hela peke yake, yani ile misingi imebadilika sana, na vitu vingi ambavyo vilikuwa vinapingwa vilionekana vya
Mwana Fa amesema mbali na ukweli kuwa muziki kwasasa umekuwa biashara lakini sio vizuri watu wasio na vipaji kuutumia kuingiza pesa na kuharibu maana ya muziki bora wafanye vitu vingine
“Muziki umekuwa biashara kiukweli, kama unaleta hela why not watu wachukue hela zao, lakini ninachopinga ni kuipoteza kabisa Hip Hop kwa sababu ya hela, kuna vitu vingi vya kufanya na bado ukapata mkate wako wa kila siku, sio lazima usingizie unafanya hii aina ya muziki tunayoifanya wakati huna talent hiyo, sio lazima kujisingizia kufanya kitu ambacho huna uwezo nacho ili tu uingize hela” Alisema Mwana FA.
No comments:
Post a Comment